Pembe ya Chifu
Leo Daly
Marleen Visser

Chifu aliyeitwa Mfupi na Duara, alilia, "Nina tatizo kubwa sana."

1

"Nimeipoteza pembe yangu inayotumika wakati wa upanzi," Chifu Mfupi na Duara alisema.

2

"Nitaipata pembe yako. Nitaenda kuitafuta nyumbani kwa Mjomba Mstatili," Jojo alisema.

3

Jojo na Mjomba Mstatili walitafuta kila mahali lakini hawakuipata ile pembe.

4

"Nenda uone ikiwa Mama Pembetatu anayo ile pembe," Mjomba Mstatili alisema.

5

Jojo alifika nyumbani kwake akanywa maji baridi kabla kuendelea na safari.

6

Jojo alimtembelea Almasi na kumwuliza ikiwa angeweza kuambatana naye.

7

"Si mbali lakini nitatayarisha chakula kidogo ili tubebe," Almasi alisema.

8

Almasi na Jojo walipumzika na kula chakula chao chini ya mlima wa pembetatu.

9

Walipokuwa wamepanda nusu ya mlima, walimwona buibui na utando wa ajbu.

10

Jojo na Almasi walifika nyumbani kwa Mama Pembetatu

11

"Chifu hakuacha pembe yake hapa," Mama Pembetatu alisema.

12

Mama Pembetatu alijua mahali wangeipata ile pembe.

13

Ilikuwa jioni walipowasili nyumbani kwa Chifu Mfupi na Duara.

14

Mama Pembetatu alimwelekezea chifu kidole. "Umeifunga pembe yako kichwani."

15

Chifu Mfupi na Duara alimpa Jojo ile pembe kuipuliza. Wote walifurahi tena.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Pembe ya Chifu
Author - Leo Daly
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Marleen Visser
Language - Kiswahili
Level - First sentences