

Hapo zamani, wanyama wa pori waliishi pamoja.
Kunguru na Mbweha walikuwa marafiki wakubwa.
Wakati huo kulitokea njaa. Wanyama hawakuwa na chakula.
Mbweha na Kunguru walienda kutafuta chakula.
Walipoipata nyama, Kunguru alianza kuila peke yake.
Mbweha alipoona hivyo, alimnyanyua Kunguru.
"Je, nikuue au la?" Mbweha alimwuliza.
"Tafadhali, usiniue! Hasa, usinitupe chini ya mwamba," Kunguru alimsihi.
Mbweha alimjibu, "Sitakutupa chini ya mwamba."
Lakini ulikuwa uongo. Mbweha alinuia kumtupa Kunguru chini ya mwamba.
Mbweha alimptupa Kunguru chini ya mwamba.
Kisha alitazama kutoka pembeni akitaka kuuona mwili wa Kunguru.
Wakati huo, Kunguru alikuwa amegeuka na kuanza kuruka hewani.
Kunguru alitua mtini.
Mbweha na Kunguru walitazamana.
"Niliepuka kwa sababu mimi ni mwerevu," Kunguru alijigamba.
"Uliepuka kwa sababu nilikuruhusu uepuke," Mbweha alimjibu.

