Ngoma
Athieno Gertrude
Salim Kasamba

Ngoma imekuwa ala muhimu ya muziki katika jamii mbalimbali. Tunazipenda ngoma!

Tuna ngoma za vimo tofauti: kubwa, wastani na ndogo.

1

Tunazicheza ngoma kwa kutumia kijiti, au kwa kutumia vidole vyetu.

Tunazicheza kwa sababu tofauti. Tunazicheza kwa nyimbo na densi, wakati wa sherehe na wakati wa majonzi.

2

Ngoma huongezea nyimbo ladha na kuwafanya watu watake kucheza. Ngoma hufanya sherehe kuwa maridadi.

Tunazicheza wakati wa harusi na tunapomtaja mtoto jina. Tunacheza kusherehekea mavuno au kuzaliwa kwa mapacha.

3

Ngoma hulia kutangaza majonzi na kuwaita watu kunapotokea kifo.

4

Ngoma hulia kuwaita watu kusafisha kisima, barabara, au kumjengea mtu mkongwe nyumba.

Ngoma hutuita ng'ombe wetu wanapokuwa wameibwa.

5

Ngoma hulia kuwaita watu wakutane kwa chifu wetu.

6

Ngoma huwaita watu kwenda kanisani kwa maombi siku ya Jumapili, na kwenye siku zingine za maombi.

Pia, ngoma huchezwa kutia ladha wimbo unapoimbwa kanisani.

7

Ngoma kubwa husikika, "An a bul mba, an a bul mba, an a bul mba-mba-mba-mba bul." Nayo ndogo hutoa sauti ya juu, "Tindiri, tindiri tindiri ti."

Pamoja zote huitikia, "Tindiri mba, tindiri mba, tindiri mba-mba-mba-mba, tindiri ti!"

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Ngoma
Author - Athieno Gertrude
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Salim Kasamba
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs