

Ngoma imekuwa ala muhimu ya muziki katika jamii mbalimbali. Tunazipenda ngoma!
Tuna ngoma za vimo tofauti: kubwa, wastani na ndogo.
Tunazicheza ngoma kwa kutumia kijiti, au kwa kutumia vidole vyetu.
Tunazicheza kwa sababu tofauti. Tunazicheza kwa nyimbo na densi, wakati wa sherehe na wakati wa majonzi.
Ngoma huongezea nyimbo ladha na kuwafanya watu watake kucheza. Ngoma hufanya sherehe kuwa maridadi.
Tunazicheza wakati wa harusi na tunapomtaja mtoto jina. Tunacheza kusherehekea mavuno au kuzaliwa kwa mapacha.
Ngoma hulia kutangaza majonzi na kuwaita watu kunapotokea kifo.
Ngoma hulia kuwaita watu kusafisha kisima, barabara, au kumjengea mtu mkongwe nyumba.
Ngoma hutuita ng'ombe wetu wanapokuwa wameibwa.
Ngoma hulia kuwaita watu wakutane kwa chifu wetu.
Ngoma huwaita watu kwenda kanisani kwa maombi siku ya Jumapili, na kwenye siku zingine za maombi.
Pia, ngoma huchezwa kutia ladha wimbo unapoimbwa kanisani.
Ngoma kubwa husikika, "An a bul mba, an a bul mba, an a bul mba-mba-mba-mba bul." Nayo ndogo hutoa sauti ya juu, "Tindiri, tindiri tindiri ti."
Pamoja zote huitikia, "Tindiri mba, tindiri mba, tindiri mba-mba-mba-mba, tindiri ti!"

