Pa Nase buibui, na wanawake
Abdul Koroma
Kenneth Boyowa Okitikpi

Hapo zamani, kulikuwa na buibui aliyeitwa Pa Nase. Alihisi njaa sana akaamua kutafuta chakula.

Alienda kwa rafikiye aliyekuwa akimpa masaada. Lakini rafikiye hakuwa nyumbani.

1

Pa Nase, alikuwa na wazo tofauti la kuweza kupata chakula. Alikumbuka kuwa mle kijijini, kulikuwa na ghala ambamo wanawake wa kijijini walikuwa wakihifadhi chakula chao.

2

Alinyatia akaingia katika lile ghala na kuiba samaki na ndizi.

3

Alipokuwa njiani akirudi, watoto waliona namna alivyotembea kwa njia isiyokuwa ya kawaida.

Wanawake walipojua, walimfuata Pa Nase kwa haraka.

4

Akiwa na mifuko iliyojaa, Pa Nase aliogopa akataka kukimbia.

Wanawake walimshika wakaamua kumuadhibu.

5

"Hebu tumsagie kwenye lile jiwe la kijijini," Yalol, mmoja wa wanawake alipendekeza.

6

Pa Nase alicheka kwa sauti akasema, "Babu yangu huishi kwenye lile jiwe. Kunisagia pale ni kama kunituma nyumbani. Asanteni!"

Wanawake waliamua kutomsaga.

7

"Tumtupe motoni," Betty akasema.

Pa Nase alicheka tena, akasema, "Bibi, yangu anayenipenda sana, ni mwenye mioto yote. Kunitupa motoni ni kama kunituma nyumbani. Asanteni!" Wanawake waliudhika sana.

8

"Tukijaze kikapu matunda, tumweke ndani kisha tukitupe mtoni," Yabana alipendekeza. Pa Nase alilia, "Mkifanya hivyo, mtaniua."

Wanawake walifurahi. Walikijaza kikapu matunda, wakamweka ndani kisha wakakitupa mtoni.

9

Pa Nase alipofika katikati ya mto, alisherehekea. Aliyachukua baadhi ya matunda na kuyala huku akiwacheka wale wanawake.

10

Wanawake wale walijua kuwa Pa Nase alikuwa amewadanganya.

Walijaribu kumnasa, lakini hawakuweza kwani Pa Nase alisombwa haraka kwa maji.

11

Pa Nase alisahau kuwa kulikuwa na wavu sehemu ya chini ya mto. Alinaswa kwenye wavu ule akawa ametegwa.

Hakuna aliyeenda kumsaidia.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Pa Nase buibui, na wanawake
Author - Abdul Koroma
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Kenneth Boyowa Okitikpi
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs