Musa na paka
Zainab Muhd Kazaure
Tawanda Mhandu

Musa anaishi na wazazi wake katika kijiji cha Mafunzo.

Yeye ni mvulana mwerevu, lakini ni kaidi.

1

Musa pia ni mchokozi. Yeye huwapiga wenzake.

Pia huwapiga wanyama anapowakuta.

2

Siku moja anapokuwa akitoka shuleni, anamwona paka.

Anambeba paka yule na kwenda naye nyumbani.

3

Babake anapomwona, anamwambia, "Musa, acha kumnyanyasa paka huyo! Mrudishe mahali ulikompata."

4

Musa anakataa kumrudisha paka alikomuokota. Badala yake, anamfungia katika ngome.

5

Musa anapolala usiku huo, anaota ndoto.

Anamwona paka akiwa mkubwa kwa umbo huku akikimbia kuelekea mahali aliko. Kinywa chake ki wazi na meno ni makali. Paka anataka kumla Musa.

6

Paka anaanza kumeza miguu ya Musa. Anaikula hadi kwenye magoti.

Kisha Musa anaamka.

7

Siku inayofuata, Musa anamrejesha paka mahali alikomuokota.

Tangu wakati huo, Musa anaahidi kuwa mvulana mzuri.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Musa na paka
Author - Zainab Muhd Kazaure
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Tawanda Mhandu
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs