

Katika mtaa wa Mfalele, kulikuwa na mvulana aliyeitwa Bobo. Aliishi na wazazi wake.
Bobo aliwaheshimu wazazi wake na watu wote mtaani kwao.
Jumatatu ni siku inayokuwa na shughuli nyingi pale mtaani. Watoto hujitayarisha kurudi shuleni baada ya wikendi.
Siku moja Bobo alipokuwa njiani kwenda shule, alikutana na rafikiye, Jeuri.
Jeuri alipenda kupigana na kuwachokoza wengine. Mara nyingi alikosa kuhudhuria shule. Alikuwa mvulana mtundu aliyecheza Kamari na kuandamana na watu wengine waovu.
Jeuri alimshawishi Bobo. Bobo hakupenda kuachwa na wavulana wengine. Polepole, alianza kuwa na tabia mbaya kama Jeuri.
Bobo alianza kuwachokoza watu. Pia, hakuwaheshimu wazazi wake na watu wengine.
Alianza kulewa akashindwa kujitunza.
Bobo hakuyajali maisha yake. Aliambukizwa ugonjwa wa zinaa. Alipoanza kukonda, Jeuri alimfanya mzaha na kuukatiza urafiki wao.
Wazazi wa Bobo walimhimiza aitembelea kliniki iliyokuwa karibu apate matibabu. Alitibiwa na akapata nafuu.
Bobo alitafakari juu ya maisha yake akaamua kubadilika. Aligundua kwamba alikuwa amefanya urafiki na adui.
Alianza kutia bidii masomoni na kuwaomba msamaha wazazi wake na walimu.
Mwanzoni, Jeuri alikasirika alipomwana Bobo akibadilika na kuwa mwema.
Baadaye, alianza kujutia tabia zake mbaya.

