Tarik na rafiki yake
Biniam Asfaw
Isaac Okwir

Tarik na familia yake waliishi mbali na mji mkuu.

1

Tarik alikuwa na mbwa aliyeitwa Buchi. 

Walikuwa marafiki wakubwa.

2

Siku moja, Tarik na rafiki yake Bedilu waliwapeleka mifugo malishoni.

3

Bedilu alipenda wacheze, lakini Tarik alitaka kusoma.

4

Mwishowe, Bedilu na Tarik waliamua kucheza.

5

Walipokuwa wakicheza, kondoo walitoweka. 

Waliwatafuta kila mahali.

6

Mbwa mwitu aliua kondoo wa Tarik.

Tarik aliogopa kuadhibiwa na baba yake.

7

Tarik aliamua kulala juu ya mti.

Buchi alilala karibu na mti huo.

8

Usiku, fisi walipiga kelele Tarik akaogopa.

9

Tarik alianguka kutoka mtini. 

Alisikia kelele karibu naye.

10

Wakati huo, radi ilimlika anga.

Tarik alimwona Buchi akiwa anamlinda!

11

Tarik na Buchi waliketi juu ya mti hadi asubuhi.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Tarik na rafiki yake
Author - Biniam Asfaw
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Isaac Okwir
Language - Kiswahili
Level - First words