Anansi mlafi
Ghanaian folktale
Wiehan de Jager

Anansi aliwakuta kunguru wakila makuyu.

Yeye pia alitaka makuyu.

1

Kunguru walimpatia Anansi makuyu.

2

Kunguru walimwambia, "Sasa njoo uchume makuyu nasi."

3

Walienda kuchuma makuyu pamoja. 

Lakini Anansi alichukua makuyu yote.

4

Anansi aliruka.

Alianguka ndani ya mto uliojaa mamba.

5

Anansi alisema, "Mimi ni mmoja wa jamaa zenu."

Hakuliwa.

6

Anansi alijifanya kuwa anakunywa maji chafu kama mamba.

7

Mamba walimwamini Anansi. 

Walimualika kukaa nao.

8

Anansi alisema, "Nitakaa, lakini, hebu kwanza niilete famalia yangu."

9

Mamba alimbeba Anansi hadi ukingo wa mto.

10

Anansi alitoroka.

Mamba bado anamsubiri hadi leo.

11
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Anansi mlafi
Author - Ghanaian folktale
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - First words