

Mbuzi alikuwa mfalme wa wanyama na ndege.
Aliita mkutano.
Mbuzi aliwaambia kwamba aliota ndoto.
Wote walisikiliza.
Ndoto ilihusu njaa.
"Tutafanyaje?" Paka aliuliza.
Kuku na Bata walisema, "Ni vyema sisi kuweka chakula kwa mfalme."
Mfalme Mbuzi alisema, "Mfunge yeyote atakayekataa kutii."
Wakati wa kumchagua mfalme mpya ulifika.
Walimchagua Paka.
Mbuzi hakutaka Paka kuwa mfalme.
"Mimi ndiye mfalme."
Mbuzi alikataa kupeleka chakula.
Ng'ombe aliuliza, "Tutafanyaje?"
Wanyama na ndege walijadili pamoja.
Walimkasirikia Mbuzi.
Mbwa alisema, "Nilikuwa naye wakati wote alipokuwa mfalme."
Kondoo akasema, "Niliwapatia watoto wake sufu yangu nyororo."
Nguruwe alilila, "Alipokuwa mfalme, nilimchungia bustani yake."
"Kwani Mbuzi alifikiri atakuwa mfalme milele?" Kondoo aliuliza.
Wanyama walikubaliana.
Lazima Mbuzi apeleke chakula kwa mfalme Paka.
Walipomkuta Mbuzi, aliwaambia, "Nitakuwa mfalme wakati wote."
Wanyama walimjibu, "Tutakufunga tukupeleke kwa mfalme mpya."
Ng'ombe alimvuta Mbuzi kumpeleka kwa mfalme.
Wengine walishangilia.
Hiyo ndiyo sababu mbuzi hukataa kusonga wanapovutwa.

