Anansi mwenye wivu
Ghanaian folktale
Wiehan de Jager

Anansi na Sungura walikuwa marafiki.

Anansi alionea wivu mali ya Sungura.

1

Anansi alimfukuza Sungura kisha akachukua shamba lake.

2

Anansi aliuza mazao yote akapata pesa nyingi.

3

Anansi alirudi nyumbani akiwa amekibeba kikapu kichwani.

4

Anansi alikiweka kikapu chini akajikinga asinyeshewe.

5

Muvua ilisababisha mafuriko hadi Anansi akajificha shimoni.

6

Tai alikiona kikapu akakifunika kwa mabawa yake.

7

"Kikapu hiki ni changu," Tai alisema.

"Ni changu!" Anansi alimjibu.

8

Tai alisema, "Nilipata mahindi na pesa hapa bila mwenyewe."

9

Chifu na wazee wake walichukua muda kuamua nani alisema ukweli.

10

Hatimaye, walisema, "Tai anasema ukweli. Kikapu ni chake."

11

Sungura alirudi katika shamba lake.

Anansi hakua na pesa wala marafiki.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Anansi mwenye wivu
Author - Ghanaian folktale
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - First words