Kima na Fisi
Mulualem Daba
Salim Kasamba

Kima na Fisi waligombana.

Walitaka ushauri wa Hakimu.

1

Hakimu aliwaza, "Kima atakula mahindi yangu. Fisi atakula mifugo wangu!"

2

Mwishowe, Hakimu aliwaambia, "Tafuteni ushauri wa wazee wa kijiji."

3

Wazee pia waliogopa.

Hawakuamua kesi kati ya Kima na Fisi.

4

Wazee waliwaambia Kima na Fisi, "Kesi hii ni ngumu sana."

5

Wazee walisema, "Tafuteni ushauri kutoka kwa mwanamke maskini."

6

Mwanamke maskini alikubali kuamua kesi yao.

"Sina mali ya kupoteza."

7

Alimwambia Fisi, "Wewe unaheshimiwa, ni mkubwa na ni shujaa. Acha ugomvi."

8

Fisi alijibu, "Umesema ukweli. Nitakomesha huu ugomvi. Sitaki aibu."

9

Mwanamke alimwambia Kima, "Wewe ni mwerevu. Acha ugomvi."

Kima alikubali.

10

Aliwaambia, "Mmekubali kukomesha ugomvi. Ni vyema kusameheana."

11

Mwanamke maskini alisuluhisha tatizo lao.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Kima na Fisi
Author - Mulualem Daba
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Salim Kasamba
Language - Kiswahili
Level - First words