

Mtu, Simba, Mbwa, Nyoka, Tai na Punda walienda vita.
Yona na mkewe waliwakaribisha kwao.
Wakawachinjia ng'ombe wao.
Kila mmoja alitaka sehemu tofauti ya ng'ombe.
Waliahidi kuwapa zawadi.
Yona na mkewe walimpa kila mmoja sehemu ya nyama aliyotaka.
Baada ya kula, walilala vizuri.
Asubuhi, walienda zao.
Wiki nyingi zilipita.
Simba akawaletea zawadi ya pembe kubwa ya tembo.
Mbwa akasema, "Zawaidi yangu itakuwa kuwachungia pembe hii ili isiibwe."
Ndugu wa Yona akawaza, "Nitaiba ile pembe niiuze."
Alipoenda kuiba ili pembe, Nyoka alimuuma.
Yona na mkewe wakachukua mifugo wa mrehemu.
Wakawa matajiri.
Tai akawaona wafanya biashara.
Walibeba pesa na vito vya bei.
Tai akazinyakua zile pesa na vito.
Akawapelekea Yona na mkewe.
Punda alichoka kumbebea tajiri wake gunia nzito la pesa.
Akawapelekea Yona na mkewe lile gunia la pesa.
"Nashukuru mlivyonisaidia."
Yona akasema, "Wanyama wametupa zawadi zao. Lakini, Mtu hajafanya hivyo."
Walingonja, wakangoja, lakini, Mtu hakuwaletea zawadi yake alivyoahidi.

