

Kijiji changu kina mbuzi.
Kiko mbali na miji mikubwa.
Mama aliniambia, "Tunakupa zawadi unaposherehekea miaka sita ya kuzaliwa."
Mimi, mama na shangazi tulisubiri basi kufika.
Mama alinipakata miguuni.
Nililala wakati wote tuliosafiri.
Tulifika sokoni.
Niliiona helikopta maridadi ya bluu.
Kibanda kimoja kilikuwa na matunda.
Nilimwuliza mama, "Haya yanaitwaje?"
Mama alijibu, "Haya ni matofaa."
"Tafadhali, ninunulie moja," nilisema.
Niliusahau mkona wa mama.
Nilizingatia tu lile tofaa langu.
Nilipomaliza kula tofaa, nilijikuta nikiwa peke yangu.
Nilianza kulia.
Mwanamke mmoja alinichukua.
Alinipeleka walikokuwa watoto wengine.
Niliwaza kuwa labda watoto waliuzwa sokoni.
Nililia zaidi.
Mwanamume aliuliza, "Elly yuko wapi?"
Nilijificha ili asinione.
Sauti ya mama niliyoijua, iliita, "Elly!"
Nilifurahi sana.
Shangazi yangu aliitoa helikopta maridadi.
"Ni yako!" alisema.

