Ujanja wa Sungura
Dan Kaasha
Abraham Muzee

Sungura alimkuta Tembo. Tembo alikuwa amekibeba chungu cha asali.

1

Tembo alimbeba Sungura mgongoni.

Sungura aliilamba asali ya Tembo.

2

Walimpata Nyati mtoni akinywa maji.

3

Sungura aliwauliza Tembo na Nyati, "Nani kati yenu aliye na nguvu zaidi?"

4

Sungura alisema kwamba alijua namna atakavyojua ukweli.

5

Kwanza, Sungura alimfunga Tembo kamba kiunoni.

6

Kisha akamfunga Nyati kamba ile ile kiunoni.

7

Sungura alijificha kwenye mti akasema, "Haya! Vuteni!"

8

Nyati na Tembo walivuta. Tembo akamvuta Nyati.

9

Nyati akamvuta Tembo.

Hakuna aliyeshinda.

10

Sungura aliikata ile kamba karibu na Nyati.

Tembo alianguka kwa kishindo!

11

Sungura alimshangilia Nyati akisema, "Ni wewe mwenye nguvu zaidi."

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Ujanja wa Sungura
Author - Dan Kaasha
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Abraham Muzee
Language - Kiswahili
Level - First words