

Sungura alikuwa amelala chini ya mti.
Tofaa likaanguka kutoka mti ule.
Sungura akasikia sauti ikisema, "Kimbia Sungura, kimbia!"
Sungura akasema, "Kitu kilianguka nikasikia, 'Kimbia Sungura kimbia!'"
Kuku alianza kukimbia aliposikia alivyosema Sungura.
Wakamwambia Mbwa, "Sungura alisikia kitu kikianguka naye akakimbia."
Mbwa akaanza kukimbia pamoja na Sungura na Kuku.
Mbwa akamwambia Farasi, "Sungura alisikia kitu kikianguka naye akakimbia."
Farasi akaanza kukimbia pamoja nao.
Punda akawauliza, "Mbona mnakimbia?"
Farasi akamjibu, "Sijui."
Punda pia akaanza kukimbia pamoja nao.
Punda akamwambia Ng'ombe, "Sungura alisikia kitu kikianguka akakimbia."
Ng'ombe alikuwa na wasiwasi.
Akaanza pia kukimbia pamoja nao.
Ng'ombe akamwambia Paka, "Sungura alisikia kitu kikianguka naye akakimbia."
Paka akaanza kukimbia na wanyama wengine.
Walimkuta mvulana akawauliza, "Kwani hamjui kilichotendeka?"
"Ni mimi niliyesema, "Kimbia Sungura kimbia!"
Mvulana alicheka.

