

Mbweha alikuwa na njaa.
Alienda kuwinda.
Alimfukuza panya.
Panya alijificha chini ya jiwe.
Mbweha alichimba kumtoa panya.
Jiwe liliangukia mguu wake.
Sungura alimsikia Mbweha akilia.
Alikimbia kuona kilichotokea.
Sungura alikubali kumsaidia Mbweha.
Mbweha aliahidi kumpatia chakula.
Sungura alilisukuma jiwe.
Liliondoka kwenye mguu wa Mbweha.
Sungura alimdai zawadi yake.
Mbweha alitisha kumla Sungura!
Walimtafuta mzee kuwaamulia kesi yao.
Mbweha alitisha kumla yule mzee pia!
Mzee alisema, "Hebu nione lile jiwe kabla kuamua."
Mbweha na Sungura walimwonyesha mzee lile jiwe.
Mbweha alieleza jinsi jiwe liliangukia mguu wake.
Mzee alimwuliza Sungura, "Nionyeshe namna ulivyolisukuma jiwe."
Sungura alilisukuma jiwe.
Liliangukia mguu wa Mbweha.
Mzee alisema, "Sasa ni sawa. Hebu twende nyumbani."
Mzee na Sungura walienda zao.
Mbweha aliachwa akiwa amenaswa.

