Magezi na Kasiira
Cornelius Gulere
Brian Wambi

Magezi na Kasiira waliishi pamoja.

Walishiriki chakula pamoja.

1

Magezi alisema, "Tulime pamoja jinsi tunavyokula pamoja."

2

Magezi alimwambia Kasiira, "Wewe lima mimi nitapanda."

3

Magezi pia alimwambia Kasiira, "Wewe panda mimi nitapalilia."

4

Mtama ulikomaa.

Kasiira alimwambia Magezi avune.

5

Magezi alijibu, "Wewe vuna. Mimi nitahifadhi."

6

Magezi alikuwa mvivu. 

Kasiira alimpatia kifungu kimoja tu cha mtama.

7

Magezi alikutana na Kuku.

8

Kuku alikula ule mtama.

Alimpatia Magezi yai.

9

Magezi aliwakuta watoto wekicheza.

Walilivunja lile yai.

10

Watoto walimpatia Magezi embe.

11

Magezi alimkuta Kasuku.

Kasuku alilikula embe kisha akampatia unyoya.

12

Ziwa liliuchukua unyoya.

Likampatia Magezi maji.

13

Magezi aliyatumia maji kuzima moto wa wachoma makaa.

14

Wachoma makaa walimpatia Magezi shoka.

15

Magezi aliwakuta wachinjaji.

Waliivunja shoka.

16

Magezi alipatiwa kichwa na mkia wa fahali. 

Ona alichofanya Magezi!

17

Alipiga mayowe, "Fahali wa mfalme amekwama matopeni!"

Ulikuwa ujanja tu.

18

Watu walikuja kumsaidia.

Magezi aliwaambia, "Vuteni mkia na kichwa."

19

Magezi aliwaambia watu, "Nipeni ng'ombe wenu nimpelekee mfalme."

20
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Magezi na Kasiira
Author - Cornelius Gulere
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Brian Wambi
Language - Kiswahili
Level - First words