Wanyama Wanatoroka kwao
Cissy Kiwanuka Luyiga
Magriet Brink

Bi kizee mmoja alikuwa na kuku na Jogoo mzee.

1

Mjukuu wake alimtembelea. Aliamua kumchinja yule Jogoo mzee.

2

Jogoo alitorokea jijini ili kujiokoa.

3

Njiani, Jogoo alimkuta Paka. Alikuwa akitoroka kutoka kwa mkubwa wake.

4

Jogoo na Paka walimkuta Mbwa akitoroka pia.

5

Farasi aliyekuwa akitoroka, alijiunga nao.

6

Wanyama hao waliwaona wezi ndani ya nyumba.

7

Walitaka kuwafukuza wale wezi. Waliimba kwa sauti ya juu.

8

Wezi walitoroka. Wanyama walikula chakula chote walichopata mle nyumbani.

9

Wezi waliamua kurudi baadaye. Lakini, wanyama waliwavamia.

10

Wezi walitoroka wakaenda zao kabisa.

11

Wanyama waliishi pamoja katika nyumba ile kwa furaha.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Wanyama Wanatoroka kwao
Author - Cissy Kiwanuka Luyiga
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Magriet Brink
Language - Kiswahili
Level - First words