

Hapo zamani, kulikuwa na nyumbu mrembo.
Aliitwa Waridi.
Farasi mwenye umbo zuri alisema, "Lazima nimwoe Waridi."
Farasi alimwambia Waridi, "Twende mtoni pamoja."
Farasi alimwuliza Waridi kuwa mke wake.
Waridi alikubali.
Farasi alitaka kumfahamu Waridi zaidi.
Alimwuliza, "Wazazi wako ni nani?"
Waridi alijibu, "Mama yangu anaishi katika ikulu ya mfalme."
"Dada yangu anaishi katika uwanja wa kanisa. Kwani humjui?"
Aliongeza, "Shangazi yangu mrembo anaishi na mzee wa kijiji."
Wakati huo, punda mzee alipita. Alikuwa babake Waridi.
Waridi hakumsalimu babake wala hakumtazama.
Punda yule mzee akauliza, "Kuna nini binti yangu?"
Farasi alimwuliza Waridi, "Huyu punda mjinga ni nani?"
Waridi alimjibu, "Mimi simjui."
Farasi alimpiga teke yule punda mzee.
Punda mzee alivunjika moyo.
Alilia kisha akafa.
Waridi hakumheshimu babake.
Hii ndiyo sababu nyumbu hawazai watoto.

