

Chura na Nyoka walikuwa marafiki.
"Njoo twende tukamtembelee mamangu." Chura alimwalika Nyoka.
"Asante, lakini nani atatuchungia makao yetu?" Nyoka alimwuliza Chura.
"Nitawachungia makao yenu," Kima alijitolea.
Chura aliweka mchwa mkobani kumpelekea mamake.
Chura na Nyoka waliondoka asubuhi wakaingia msituni.
Waliwakuta vichakuro. Nyoka aliwaogopa.
Chura alimlinda rafiki yake Nyoka.
Walipofika kwa mamake Chura, walikuwa wakihisi njaa sana.
Walinawa wakajitayarisha kwa chakula.
"Nyoka, tafadhali keti wima." Chura alimwambia rafikiye.
Nyoka alijaribu kuketi wima, lakini hakuweza. Yeye si kama chura.
"Siwezi kuketi wima kama chura," Nyoka alimjibu.
Chura hakumsikiza Nyoka. Alianza kukasirika.
Nyoka pia alikasirika akasema, "Hunielewi. Heri nirudi nyumbani."
Nyoka aliondoka kwa hasira. "Nilidhani Chura ni rafiki yangu." Aliwaza.

