Sokwe na Mamba
Mulualem Daba
Abraham Muzee

Sokwe alimkuta Mamba kando ya ziwa.

1

Akamwuliza Mamba, "Unaishi wapi?"

Mamba akamjibu, "Ziwani."

2

Mamba akamwuliza, "Wewe unaishi wapi?"

Sokwe akamjibu, "Kwenye miti."

3

Mamba akataka kumjua Sokwe zaidi.

Akamwuliza, "Unaweza kuogelea?"

4

"Siwezi," Sokwe akamjibu.

Mamba akasema, "Nitakufunza."

5

Mamba akasema, "Sisi sasa ni marafiki. Usiogope."

6

Mamba akasema, "Mjomba ni mgonjwa. Anahitaji
nyama ili apone."

7

Sokwe akaogopa sana.

Je, Mamba atamula?

8

Sokwe akataka kumtoroka Mamba.

9

Sokwe akapata wazo zuri.

10

"Nitautoa moyo wangu umpatie," Sokwe akaahidi.

11

"Lakini moyo wangu uko mtini," Sokwe akasema.

12

"Utauleta moyo wako?" Mamba akauliza.

Sokwe akamjibu, "Ndiyo."

13

Mamba akaogelea kutoka majini.

Sokwe akakimbilia kwenye miti.

14

"Wewe si rafiki yangu. Ulinidanganya!" Mamba akasema.

15

"Hatuko marafiki. Unataka kunila!" Sokwe akamjibu.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Sokwe na Mamba
Author - Mulualem Daba
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Abraham Muzee
Language - Kiswahili
Level - First words