Musau na babake
Kanyiva Sandi
Benjamin Mitchley

Musau aliishi na babake, Syonzola.

1

Syonzola alienda kunywa pombe kila siku.

2

Aliporudi nyumbani, aliita, "Njooni mnisaidie! Nauawa na fisi."

3

Watu waliitikia mwito wake.

Lakini, fisi hakuwepo.

4

Syonzola alifanya hivyo kila usiku.

5

Musau aliamshwa na kelele za babake.

6

Fisi alimvamia Syonzola usiku mmoja.

Syonzola alilia, "Nisaidieni!"

7

Watu walisema, "Syonzola ametuchosha. Ni uongo wake wa kawaida."

8

Musau alisubiri.

Babake hakufika.

9

Musau aliwaza, "Labda babangu yuko hatarini."

10

Musau alitoka nje mbio.

11

Aliita, "Baba! Baba!" 

Fisi alikuwa akimvuta babake mguu.

12

Kutoka siku hiyo, Syonzola alibadilika.

Anawasimulia watoto hadithi.

13
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Musau na babake
Author - Kanyiva Sandi
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Benjamin Mitchley
Language - Kiswahili
Level - First words