Jinsi usiku ulivyoingia kijijini
Robert Ekuka
Wiehan de Jager

Opio aliishi katika kijiji kisichokuwa na majira ya usiku.

Watu walipochoka, walilala na kufanya kazi walipoamka.

1

Siku moja Opio na mbwa wake walienda kuwinda. Mbwa walimfukuza paa naye Opio akawafuata.

Mwishowe, hakuwaona tena.

2

Opio alikimbia mpaka akachoka.

Alikaribishwa na mtu mmoja aliyempa kileo kunywa.

3

Opio alipoamka, hakuweza kuona.

Alimlalamikia mwenye nyumba, "Ulininywesha nini? Mbona sioni tena?"

4

Mwenye nyumba alimwambia Opio, "Sasa ni usiku. Kwani hujui usiku?" 

Opio aliuliza maswali mengi kuhusu usiku na mchana.

5

Asubuhi, Opio alielezwa jinsi ya kuupeleka usiku kijijini kwao.

Aliambiwa atembea kuelekea kwao bila kutazama nyuma.

6

Usiku huo Opio alisafiri kwenda kijijini kwao akifuatwa na giza.

Hakutazama nyuma.

7

Alipofika kijijini kwao, wanakijiji waliogopa wakamwuliza, "Hiki ni kitu gani cheusi kilichokufuata?"

Opio aliwaeleza, "Hili ni giza la usiku. Mwangaza huwa mchana."

8

Opio aliendelea kuwaeleza, "Tutafanya kazi mchana na usiku tutapumzika."

9

Na hivyo ndivyo usiku ulivyoingia katika kijiji cha kina Opio.

10
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Jinsi usiku ulivyoingia kijijini
Author - Robert Ekuka
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - First sentences