Fisi mlafi
John Nga'sike
Salim Kasamba

Hapo zamani, kulikuwa na dada wawili, Kalio na Akiru.

Siku moja, walienda kuchota maji mtoni.

1

Walipokuwa wakirudi nyumbani, waliketi juu ya jiwe kubwa kupumzika.

2

Baada ya kupumzika, Kalio hakuweza kusimama tena.

Alikuwa amekwama kwenye jiwe.

3

Akiru alikimbia nyumbani kumjulisha mama yao.

Kalio aliposubiri usaidizi, Fisi alijificha nyuma ya jiwe akimmezea mate.

4

Mama alipofika, alijaribu kumvuta Kalio, lakini ilikuwa bure.

Kalio alikuwa kweli amekwama kwenye jiwe.

5

Mama alimtuliza Kalio akisema, "Nitazungusha ua hapa ili uwe salama."

6

Mama alijenga ua.

Aliweka mlango karibu na Kalio ili autumie akimletea chakula.

7

Mama alipomaliza kujenga ua, alimwambia Kalio, "Nitakapokuletea chakula, nitakuwa nikiimbia wimbo kujitambulisha. Utakapousikia, utanifungulia."

8

Mama aliongeza kumweleza Kalio, "Usimfungulie mtu mwingine."

Mama aliimba wimbo huo kila alipokuja kumwona Kalio.

Kalio angeufungua mlango na kupatiwa chakula.

9

Fisi alijificha kila wakati akimsikiliza mamake Kalio akiimba.

10

Fisi alifanya mazoezi mengi akiiga sauti ya
mamake Kalio.

Mwanzoni, hakufaulu.

11

Wanyama wenzake walimshauri Fisi, "Mmeze nzi wa mtoni ili sauti yako iwe bora."

Fisi alimmeza nzi wa mtoni akaenda kuimba, lakini Kalio hakuufungua mlango.

12

Fisi alishauriwa na wenzake tena, "Labda ukimmeza nzi kutoka sehemu tambarare, utaimba vizuri."

Fisi alifanya alivyoshauriwa na wenzake.

13

Mara hii, sauti ya Fisi ilikuwa bora alipoimba.

Kalio aliufungua mlango na Fisi akamla.

14

Mama alimpelekea Kalio chakula kama ilivyokuwa kawaida.

Aliimba mara nyingi, lakini mlango haukufunguka.

Aligundua kwamba alikuwa amempoteza bintiye.

15

Mama alifanya mkutano na wanyama wote.

Baada ya kuwasha moto mkubwa, aliwaambia, "Nyote mtauruka moto huu. Aliyemla Kalio, ataanguka ndani na kuteketea."

16

Wanyama wengine waliuruka moto salama, mmoja baada ya mwingine.

Ilipofika zamu ya Mbweha, alisita kidogo.

17

Hatimaye, Mbweha alipouruka, moto uliiunguza ncha ya mkia wake.

Mbweha alikuwa ameionja damu ya Kalio.

18

Fisi alikuwa wa mwisho.

Alipouruka moto, alianguka ndani na kuanza kuteketea.

19

Wanyama walifahamu kuwa Fisi ndiye alikuwa amemla Kalio.

Waliimba wimbo wa kumsuta Fisi.

20
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Fisi mlafi
Author - John Nga'sike
Translation - Translators without Borders
Illustration - Salim Kasamba
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs