Tembo na Kinyonga
Stella Badaru
Wiehan de Jager

Hapo zamani katika ikulu kubwa, paliishi mfalme na bintiye mrembo.

1

Tembo aliishi katika nyumba upande mmoja wa ikulu.

Kinyonga aliishi upande mwingine.

2

Wakati huo, kukashuhudiwa kiangazi kikubwa katika nchi ile.

Mfalme alikuwa na wazo kisha akawaita majirani zake kwenda ikuluni.

3

Mfalme aliwaambia Tembo na Kinyonga, "Ninataka mkanyage ardhi hadi maji yapatikane."

Mfalme aliahidi kuwa atakayefaulu atamwoa bintiye wa kifalme.

4

Kinyonga hakuwa na matumaini yoyote kwa ajili ya udogo wake.

Tembo alifurahi mno kwani alikuwa na umbo kubwa na mwenye nguvu. Alienda uwanjani na kuanza kukanyaga aridhi.

5

Vumbi nyingi ilitokea, lakini hapakuwa na maji.

Tembo alikanyaga aridhi hata karibu maji yatokee, lakini alielekea kuchoka.

Alimwachia Kinyonga nafasi kujaribu.

6

Kinyonga alianza kukanyaga aridhi. Baada ya muda mfupi, maji yalitoka.

Watu hawakuamini macho yao!

7

Kwa hivyo, Mfalme alimpa Kinyonga bintiye.

Tembo alienda nyumbani kwa hasira.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Tembo na Kinyonga
Author - Stella Badaru
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs