

Hapo zamani katika ikulu kubwa, paliishi mfalme na bintiye mrembo.
Tembo aliishi katika nyumba upande mmoja wa ikulu.
Kinyonga aliishi upande mwingine.
Wakati huo, kukashuhudiwa kiangazi kikubwa katika nchi ile.
Mfalme alikuwa na wazo kisha akawaita majirani zake kwenda ikuluni.
Mfalme aliwaambia Tembo na Kinyonga, "Ninataka mkanyage ardhi hadi maji yapatikane."
Mfalme aliahidi kuwa atakayefaulu atamwoa bintiye wa kifalme.
Kinyonga hakuwa na matumaini yoyote kwa ajili ya udogo wake.
Tembo alifurahi mno kwani alikuwa na umbo kubwa na mwenye nguvu. Alienda uwanjani na kuanza kukanyaga aridhi.
Vumbi nyingi ilitokea, lakini hapakuwa na maji.
Tembo alikanyaga aridhi hata karibu maji yatokee, lakini alielekea kuchoka.
Alimwachia Kinyonga nafasi kujaribu.
Kinyonga alianza kukanyaga aridhi. Baada ya muda mfupi, maji yalitoka.
Watu hawakuamini macho yao!
Kwa hivyo, Mfalme alimpa Kinyonga bintiye.
Tembo alienda nyumbani kwa hasira.

