Siku ambayo Jua lilipotea
Khothatso Ranoosi
Jesse Breytenbach

Mama Jua alimtembelea dadake Mwezi. 

"Nitarudi hivi karibuni," alisema.

1

Mama Jua alipoondoka, Milima ilihuzunika.

2

Upepo uliitikisa Miti. 

Miti ikadondosha majani yake kwa hasira.

3

Anga lilianza kulalamika.

Lilibadilika na kuwa rangi ya kijivu.

4

Mawingu yalihuzunika.

Yalilia machozi mengi.

5

Ulimwengu mzima ukaanza kuzama majini.

6

Mama Jua alimbusu dadake Mwezi.

Alimuaga akiwa tayari kurejea duniani.

7

Anga lilifurahia Mama Jua.

Lilikuwa rangi ya bluu.

Milima ilitabasamu.

8

Upepo ulitulia.

Miti ikanyoosha matawi yake na kutabasamu.

9

Mawingu yalifurahi tena kumwona Mama Jua.

Yalienda kucheza.

10

Miche ilichipuka ardhini na kusema, "Hamjambo!"

Dunia nzima iling'ara.

11

Mama Jua aliangaza.

Alitabasamu akasema, "Niliwaahidi kuwa nitarejea."

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Siku ambayo Jua lilipotea
Author - Khothatso Ranoosi, Marion Drew
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Jesse Breytenbach
Language - Kiswahili
Level - First words