

Hapo zamani za kale, palikuwa na mtu aliyekuwa akitembea kichakani.
Ghafla, alimkuta Simba!
Ulikuwa msimu wa baridi.
Simba alikuwa akipumzika kwenye nyasi fupi.
Makutano hayo yalitokea ghafla mtu huyo asijue la kufanya.
Alijawa na woga.
Mwanzoni, Simba pia alishangaa na kuogopa kidogo.
Lakini, mngurumo mkubwa ulisikika kutoka tumboni mwake kwani alikuwa na njaa.
Mtu yule alijikuta juu ya mti mrefu.
Alianza kupiga mayowe.
Simba alilala chini ya mti akisubiri mlo.
Muda ulipopita, Simba alijifanya kuwa analala usingizi.
Muda mfupi baadaye, mtu yule alilala usingizi.
Aliamka tena na mwishoni alisinzia na kulala fofofo.
Aliporomoka kutoka juu na kumwangukia yule Simba aliyelala.
Wote waliamka wakiwa wamechanganyikiwa na kuogopa.
Simba alisahau mlo wake na kukimbilia usalama wake.
Mtu yule alianza kukimbia akielekea upande mmoja na Simba.
Aligundua kwamba alikuwa akikimbia na Simba!
Kwa hivyo alibadilisha mwelekeo wake na kuepuka kuliwa na Simba!

