

Mama aliziweka nguo zake katika begi ndogo.
Kisha, aliniita.
Alinikumbatia na kusema, "Kwa heri kwa sasa binti yangu."
Nilishangaa sana.
"Unaenda wapi, mama?"
Nilimwuliza nikiwa na wasiwasi.
Nilianza kulia nikitaka kumfuata. Lakini, baba alinibeba juu begani kwake.
Nililia kwa sauti lakini wapi!
Baba alisema, "Mamako anaenda hospitalini kujifungua mtoto."
Niliposikia "mtoto", nilitulia na kumwangalia baba. "Kwa nini ajifungulie hospitalini?"
Nilitaka majibu ya haraka.
Baba alinikalisha juu ya kiti kidogo na kusema, "Nitakueleza kwa nini ni lazima aende hospitalini."
Nilihuzunika.
Nilisikiliza kwa makini. Lakini sikuelewa kwa nini mwuuguzi hakuja nyumbani.
Alipomaliza, nilimwuliza, "Ataendelea kunipenda hata baada ya kurudi na mtoto mwingine?"
Babangu alinibeba na kuniambia, "Tutakupenda wakati wote."
Nilifurahi sana.
"Ninaweza kumwandikia barua akiwa huko?" Nilimwuliza baba.
Jioni hiyo, nilianza kumtungia mama barua.
Ilikuwa fupi.
Nilirarua karatasi kutoka daftari langu na kuanza kuandika.
Mama, mama, baba alisema kwamba umeenda kumleta mtoto mwingine?
Tafadhali, fanya upesi urudi nyumbani. Ninakuhitaji.
Ningependa umlete mtoto msichana ili niweze kucheza naye akiwa mkubwa.
Yeye nami tutakusaidia kazi zote.
Unaweza kuleta wawili ili mmoja awe wangu ili nimpambe.
Ninakusubiri hapa nyumbani.
Nitakulaki ukifika.
Niliikunja barua yangu ili baba ampelekee mama.
Nilipoamka asubuhi, barua haikuwapo.
Nikajua baba ndiye aliyeichukua.

