

Kasembo na wazazi wake waliishi maisha ya uchochole. Kasembo hakuweza kwenda shule ingawa aliamini kuwa ataenda siku moja.
Wanakijiji walipendezwa na urembo na ukakamavu wa Kasembo.
Kila siku Kasembo aliamka asubuhi kwenda mawindoni.
Wanakijiji walishangazwa sana na mazoea hayo.
Siku moja, Kasembo alibahatika kwa njia ya pekee.
Alifanikiwa kupata sungura mwitu.
Alitafuta kuni ili ampike yule sungura.
Aliona kijisanduku kidogo kilochokuwa kimefichwa.
Kasembo aliamua kukifungua ili kuona kilichokuwa ndani. Alipigwa na butwaa kuona dhahabu.
Alifurahi sana. Alikifunga, kisha akakibeba hadi nyumbani.
Mara moja, yeye na wazazi wake, walianza kutafuta mnunuzi wa ile dhahabu.
Walimkumbuka Kigunda, tajiri mmoja aliyehusika na biashara ya madini.
Kigunda alinunua ile dhahabu yote.
Kasembo alipata pesa za kutosha. Aliwajengea wazazi wake nyumba mpya na kuwanunulia gari.
Pesa zilizobaki, aliitumia kununua sare za shule, na kulipa karo ya miaka kadhaa.
Maisha ya Kasembo na wazazi wake ilibadilika kweli kweli.

