

Mvua ilikuwa imenyesha kwa siku nyingi na watu walikuwa wemenuna, ila Samweli, aliyeamka kila asubuhi akitabasamu.
Bibi alisema, "Eee, Samweli! Hilo tabasamu ni la ajabu! Je, ni kwa ajili yangu?"
Samweli alipiga makofi kisha akasema, "Lakini ni tabasamu langu, Bibi."
Mama alicheka. "Samweli! Tabasamu ni kitu unachoweza kupatiana bila kupotesa. Tazama!"
Mama akamnyanyua na kumupandisha mpaka kwenye kioo. Tabasamu lake lilikuwa wazi na la kuangaza kama hapo awali.
Ikafika saa ya kuondoka. Mama akafunga koti la Samweli la mvua mpaka juu. Wakaingia kwenye mvua kuelekea maktabani.
Rafiki mmoja wa Samweli aliitwa Zawadi. Alikuwa amesimama dirishani akitazama mvua bila furaha.
Samweli akahisi tabasamu likipanda ndani mwake, kisha likaruka na kuvuka bustani hadi kwa Zawadi.
Zawadi alishikilia lile tabasamu kwani lilikuwa na thamani sana asingaliruhusu liondoke. Samweli alipotembea kuelekea maktabani, aliisikia kengele mlangoni kwa Zawadi. Mtu wa barua alikuwa akimletea Zawadi barua kutoka kwa binamu yake mpendwa.
Zawadi alifurahi sana mpaka tabasamu lake likapanda juu na kumwangaza mtu yule aliyeleta barua. "Asante sana Bwana!" alisema.
Tabasamu la Zawadi lilikuwa kitu muhimu sana alichokuwa ameona mwanamume yule asubuhi nzima. Lilimpa joto alipotembea kwenye mvua.
Akafika kwenye jumba kubwa. Nyuma ya lango, kulikuwa mbwa aliyekuwa akizunguka zunguka na kubweka mfululizo. Ukali wake ulimfanya mtu yule atabasamu.
Mbwa alinyamaza kubweka. Alitega masikio na kutikisa mkia wake kisha aligeuka na kukimbia kwenda nyumbani kwa furaha.
Mzee mkongwe alifungua mlango. "Aa, la! Huwezi kuingia. Umeloa maji!" mzee alimwambia mbwa wake. Lakini, mara moja, tabasamu likamwangaza yule mzee.
Mzee alisimama wima kidogo. "Eee, nani anajali ikiwa kunanyesha? Twende matembezi, rafiki yangu!"
Wakaenda wakiruka vitimbwi vya maji. Kwenye kivuko, palikuwa na polisi wa trafiki wa kike. Alihisi baridi na kusononeka.
Mzee huyo alijua la kufanya, "Hujambo Bi Makabela!" alisema, kisha akatabasamu. Lakini, Makabela hakutabasamu hata kidogo.
Kusimama siku nyingi kwenye mvua kunaweza kufanya uso kuhuzunika sana.
Lakini tabasamu ni kitu cha ajabu, na kwa sasa, tabasamu la Bi Makabela lilikuwa kubwa, la kuangaza, na ilikuwa vigumu kulifungia ndani.
Halikufanya kazi mara moja, lakini kidogo kidogo, lilianza kutambaa hadi, mwishowe!
Tabasamu kubwa na la ajabu liliuangaza uso wa Makabela!
Kengele ya shule ilisikika, na watoto walikimbia kuvuka barabara. Bi Makabela aliiweka alama yake, kisha akatabasamu, akatabasamu, akimlenga kila mtoto.
Watoto walitabasamu walipowaona mama na baba zao, bibi zao, shangazi zao na kaka na dada zao.
Walitabasamu walipomwona dereva wa basi na muuza mboga, na Mama Makau, ambaye alitabasamu alipomwona mumewe, naye alitabasamu mbele ya meya.
Tabasamu ziliruka na kung'ara na kung'aa mpaka kila MTU akatabasamu na kuchekacheka na kucheka kwa sauti ya juu kwenye mvua.
Katika maktaba, kila kitu kilikuwa kimya isipokuwa sauti ya mvua.
"Ni wakati wa kwenda," mama Samweli alisema, huku akifunga kitabu chake.
"Ndiyo, mama!" Samweli alisema akiwa ameishiwa na tabasamu.
Lakini walipoingia kwenye barabara, ilikuwa ajabu ilioje!
Kila mtu kutoka mjini alikuwepo! Kila mtu! Na WOTE walikuwa wakitabasamu!
Tabasamu zilizunguka na kumlenga Samweli. Zilimpasha joto, na kumfurahisha, na kumpaa juu, juu, kutoka kwenye vidole vyake vya miguu hadi JUU ya kichwa chake. Alijawa na furaha kiasi kwamba tabasamu lilipasuka, nyororo na kung'aa.
Na kitu kimoja kilibadilika. Alasiri ya giza na mvua haikuonekana kuwa giza tena. Je, inaweza kuwa? NDIYO! Mawingu yaligawanyika, na jua kali likaangaza juu yao, na tabasamu kubwa zaidi, angavu zaidi kuliko yote.


