

Kwa ajili ya watoto katika kila nchi ya Afrika
Siku moja, dada yangu Zena alikuwa na wazo hili.
"Nitatengeza barakoa kwa kila asiyekuwa nayo kwenye jamii!" alisema.
"Hilo ni wazo zuri! Wacha tuwaambie Mama na Baba watakaporudi nyumbani!" nilijibu.
Mama na Baba waliporudi nyumbani, tuliwaambia kuhusu wazo la Zena.
"Hilo ni wazo zuri mwanangu!" Baba alisema, na Mama akakubali.
"Nitawauliza washiriki wa kanisa letu watupe vitambara vikusaidie kutengeneza barakoa. Hebu tumwulize Bibi asaidie pia."
Siku iliyofuata wanawake wa kanisa walituletea vitambara vya rangi nyingi na mpira nyumbani kwetu.
Zena alimuachia Bibi mfuko wa vitambara nje ya mlango wake pamoja na barua ya kumuomba amsaidie.
Zena alianza kushona barakoa, mimi na Ndolo tukamtazama.
Zena ni hodari sana kwa kushona. Alishona barakoa nyingi.
Mimi na Ndolo tulihesabu barakoa, 1, 2, 3, 4, 5 halafu 20, 30, 40, 50, halafu,100!
Zena na Bibi walishonea jamii barakoa nyingi!
Tuliwasaidia!
Mama na baba walikuwa wenye fahari.
Siku iliyofuata, Baba na Mama hawakuenda kazini. Waliamua kugawanya barakoa nzuri za Zena na Bibi kwa wale ambao hawakuwa na barakoa.
Zena alibeba sanitaiza ya Mama na kuwanyunyuzia watu. "Kumbuka kuosha barakoa yako kila siku," Mama alisema.
Sasa Zena anapoenda kuchota maji, kila mtu amevaa barakoa.
Kila mmoja anaonekana yuko salama.
Baadaye, Mama aliuliza, "Wanangu, tunafanya nini baada ya kugusa kitu chochote?"
"Tunaosha mikono yetu kwa maji na sabuni!" Ndolo alisema. "Au tunatumia sanitaiza," niliongeza.
Mama alitabasamu, "Na tunavaa nini tukienda nje?" Sote tulipiga kilele, "Barakoa zetu!"
1. Osha mikono yako kwa maji.
2. Tumia sabuni kuosha mikono yako.
3. Osha kwa sekunde 20 au polepole hesabu kutoka 1 hadi 20.
4. Suuza mikono yako kwa maji.
5. Kausha mikono yako kwa taulo au tishu safi.
6. Sasa mikono yako ni safi!

