Mtende
Simon Ipoo
Rob Owen

Hebu nikueleze kuhusu mtende.

1

Mtende ni mmea wa kudumu. Unaweza kusitawi wakati mimea yote mingine imekauka.

2

Kivuli cha mtende kina upepo mzuri.

3

Tunakula matunda ya mtende.

4

Tunatumia majani ya mtende kuezeka nyumba zetu.

5

Tunatengeneza fagio na kusuka mikeka kwa kutumia majani ya mtende.

6

Tunatumia nafaka zake kupika.

7

Sasa umefahamu kwa nini mtende ni muhimu sana?

8

Maswali: 1. Kweli au sio kweli? A)Mtende unahitaji maji mengi kusitawi. B) Mtende unatoa kivuli kizuri. 2. Jaza nafasi zilizo wazi. A) Tunatumia _____ya mtende kuezeka nyumba zetu. B) Tunasuka ________ kwa kutumia majani ya mtende. 3. Taja jina la aina nyingine ya mti inayosaidia jamii yenu. Eleza sifa zake.

9
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mtende
Author - Simon Ipoo
Adaptation - Translators without Borders, Monica Shank
Illustration - Rob Owen
Language - Kiswahili
Level - First sentences