

Musau aliishi na babake, Syonzola.
Syonzola alienda kunywa pombe kila usiku.
Aliporudi nyumbani, aliita, "Nisaidieni! Fisi ananiua."
Watu walipokimbia kumsaidia, hawakumwona fisi.
Syonzola alifanya hivyo kila usiku.
Kila mara, Musau aliamshwa na kelele za babake.
Fisi alimvamia Syonzola usiku mmoja.
Kama kawaida, Syonzola aliita, "Nisaidieni!"
Lakini watu walisema, "Tumechoshwa na Syonzola. Anatudanganya tu."
Musau alingoja. Babake hakufika.
Musau aliwaza, "Labda ni kweli kuwa babangu yuko hatarini."
Musau alitoka nje mbio.
Aliita, "Baba! Baba!" Fisi alitoroka.
Kutoka siku hiyo, Syonzola alibadilika.
Anawasimulia watoto hadithi.
Maswali: 1. Musau aliishi na nani? 2. Syonzola aliwadanganya wanakijiji kwa kufanya nini? 3. Kwa nini watu hawakumsaidia Syonzola alipovamiwa na fisi? 4. Hadithi hii inaonesha madhara gani ya pombe? Pombe ina madhara gani ambayo hayajaoneshwa katika hadithi hii?

