

Babangu alinibeba katika gari letu kwenda mjini.
Nilitazama nje ili niyafurahie mazingira yangu.
Nilimwona mwanamke aliyevaa nguo ya rangi ya chungwa.
Alikuwa akitembea kwa kasi.
Alikuwa amefunga kiunoni mshipi mkubwa mwekundu.
Mkononi, aliubeba mkoba wa rangi ya chungwa.
Miguuni, alivaa viatu vya rangi ya chungwa.
Vilikuwa na visigino virefu.
Alisimama na kuzigusa nywele zake refu.
Zilikuwa zimebanwa katikati na kibano cha rangi ya chungwa.
Alipokuwa akirekebisha kibano cha nywele, mkoba wake ulianguka chini.
"Uuui," nilisema huku nikimhurumia.
Aliinama kuuokota mkoba wake ulioanguka.
Nilitazama nguo, mshipi, viatu na mkoba.
Niliviona vipuli virefu vikubwa vya rangi ya chungwa.
Vilitikisika alipofuta vumbi kutoka kwenye mkoba.
Tulipoendelea na safari yetu, nilizidi kumtazama yule mwanamke.
"Unatazama nini?" Babangu aliniuliza.
"Mwanamke yule mrembo," nilimjibu baba.
Nilifikiria juu ya rangi tofauti na jinsi zinavyopendeza.

