Mvulana asiyetii
James Elim
Wiehan de Jager

Kijiji kimoja kilikuwa karibu na msitu.

1

Msitu huo ulikuwa na fisi na wanyama wengine wakali.

2

Watu wengi walivamiwa na fisi.

3

Ekeno alionywa na wazazi asiende mbali na nyumbani.

4

Ekeno alipuuza ushauri wa wazazi. Siku moja alienda kutafuta asali.

5

Alitembea kwa muda mrefu. Alijipata akiwa mahali asikokujua.

6

Usiku, alitafuta mahali pa kulala.

7

Usiku wa manane, Ekeno aliamua kuitafuta njia ya kurudi nyumbani.

8

Alivamiwa na fisi wakamla.

9

Wenzake walienda kumtafuta.

10

Jirani mmoja aliwaelekeza kuwa Ekeno aliingia msituni.

11

Waliamini kuwa alikuwa ameliwa na fisi.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mvulana asiyetii
Author - James Elim, Joseph Opilo
Illustration - Wiehan de Jager, Benjamin Mitchley, Catherine Groenewald, Padmanabha
Language - Kiswahili
Level - First words