Penseli ya Miujiza: Jamii ya Ndoto Zetu Temeke
Klabu ya Hadithi Zetu-Temeke Klabu ya Hadithi Zetu-Temeke

Kitu ninachokitamani katika jamii yangu ni kila mtu awe na nyumba yake kwa sababu watu wanateseka na kunyanyaswa na wenye nyumba wao. Mtu kama hana kodi, anaweza kufukuzwa kwa kudhalilishwa mbele za watu.

1

Suluhisho
Natamani serikali iwape watu ajira za kutosha ili wapate fedha za kodi au wajenge nyumba zao wenyewe ili kusiwe na mateso na kudhalilika tena.

2

Ninatamani jamii ya ndoto yangu iwe na ushirikiano kwa kila kitu; pakiwa na misiba, shughuli kama harusi au ugonjwa tusaidiane.Kitu kinachonikwaza ni wizi. Watu wanakuibia, wanakupiga na kukuacha ufe. Inaniumiza sana.

3

Nitatumia penseli ya maajabu kuondoa wizi na roho mbaya. Ndoto yangu ni kuona watu wakishirikiana kufanya usafi wa mazingira shuleni na nyumbani.

4

Nataka jamii yenye ujenzi wa nyumba nyingi za udongo, upandaji miti, na wasichana wasinyimwe haki ya kwenda madrasa.Katika jamii yangu kuna uhaba wa nyumba zenye umeme na madrasa.

5

Inanikwaza kuona wavulana wanapelekwa madrasa lakini wasichana wanabaki kufanya kazi za nyumbani.
Nimechora nikiwasilisha malalamiko yangu serikalini. Natamani serikali itujengee nyumba bora za udongo zenye umeme wa kutosha.

6

Ninatamani kuona jamii inatunza mazingira ya barabarani na sokoni kwa kuchoma na kufukia takataka.Inanikwaza kuona familia nyingi, ikiwemo yangu, hazitoi mgawanyo sawa wa kazi. Wasichana wanachoka sana.

7

Nitatumia kalamu ya miujiza kuishauri jamii yangu wavulana na wasichana wafanye kazi kwa pamoja kwa usawa bila kujali jinsia ili sote tupate muda wa kupumzika.

8

Natamani jamii inayofuata sheria, mwizi akikamatwa apelekwe polisi apate adhabu.Wizi unaharibu maisha ya watu hasa kwa wale wanaoibiwa wanarudi nyuma kimaisha pia wezi wanaweza kufa kwa kupigwa. Pia inakwaza kuona wadada wanajiuza mitaani.

9

Ndoto yangu ni kuona watu wanaacha nguo zao wanazofua nje bila kuibiwa, na wasichana wanaenda shule kutimiza malengo yao badala ya kujiuza miili yao ili kupata maisha mazuri.

10

Natamani jamii yenye upendo na kuthaminiana; kwenye mchoro wa ndoto yangu mlemavu anasaidiwa kurudi na kupelekwa nyumbani na mwanafinzi mwenzake baada ya kutoka shule.

11

Miundombinu mibovu inasababisha ajali. Inanikwaza sana kuona barabara mbovu katika makazi yetu.Ombi langu kwa serikali ni kutengeneza miundombinu mizuri kila sehemu ili watu, mimea, na wanyama wanufaike na kuepuka ajali.

12

Mchoro wa changamoto ya nyumba za kupanga
Wapangaji wanasumbuka na choo, vyumba vidogo, na migogoro ya kulipia umeme. Wapangaji wengine ni wagumu kulipa hela za umeme. Changamoto hizi za nyumba zinanikwaza sana.

13

Suluhisho
Nimechora jamii yenye wajenzi wengi. Natamani wanafunzi wasome kwa bidii wawe wajenzi ili kila familia iwe na nyumba yake na kusiwe na kero za kupanga.

14

Ninatamani jamii inayoshirikiana kufanya usafi wa mazingira yanayotuzunguka.Watu wanatupa taka ovyo na inanichukiza sana. Tusipotunza mazingira tutapata magonjwa kama vile kipindupindu na kuharisha damu.

15

Nimechora msichana akifanya usafi. Nitaiomba serikali ichukue hatua kali kwa wanaotupa taka ovyo.

16

Natamani wanafunzi waende shule na wazazi wawahudumie watoto wao vizuri. Uchafuzi wa mazingira unaleta kipindupindu na ni kikwazo kikubwa katika jamii yetu ya Temeke.

17

Kwakutumia penseli yangu ya miujiza naiona jamii ya ndoto yangu ni safi, imepandwa miti na maua, na kila mtoto msichana na mvulana anapata haki ya elimu.

18

Natamani maisha mazuri ambapo watoto wanaenda shule na wazazi wanafanya kazi.Katika jamii yetu ya Temeke tuna shida ya maji; mabomba ni machache na watu wanagombania maji yakikatika. Pia wizi wa mabomba unanikwaza.

19

Mchoro wangu unaonyesha watu wakishirikiana kujenga msikiti. Natamani tushirikiane hivyohivyo kuandika na kupeleka hoja serikalini ili tupate mabomba ya maji.

20

Inanikwaza kuona watu wanawabagua walemavu na kufanya wizi Temeke.Natamani tupendane na kusikilizana kwenye shida na raha.Nitatatua hili kwa kuwashauri watu wasiibe na wasibague walemavu ili tuwe na umoja.

21

Natamani jamii ya Temeke iwe na maktaba na pia kwa kutumia penseli ya miujiza jamii yangu ya Temeke iwe na ushirikiano na tuwe tunasikilizana kwa kila jambo.Kwenye mchoro huu watoto wakiwa nyumbani wanasoma kwa pamoja bila ubaguzi wowote.

22

Ninatamani wanafunzi wote waende shule kutimiza malengo yao.Inanikwaza kuona wavuta bangi wakibaka wasichana na kuwaharibia ndoto zao.

23

Nimechora wanafunzi wakisoma kwa amani. Nitaenda dawati la jinsia kutoa taarifa ili wabakaji wapewe adhabu kali na wasichana walindwe.Jamii ya ndoto yangu ni kuona wanafunzi wote wanasoma na kufikia ndoto zao walizozipanga.

24

Jamii ya ndoto yangu ni watoto wote, wavulana kwa wasichana, waende shule bila kuzuiliwa na wazazi.Inanikwaza kuona watu wanatupa taka sehemu zisizo rasmi na kuharibu mazingira.

25

Nimechora jamii inayotunza mazingira na kutupa taka sehemu rasmi kwa sababu tukitunza mazingira, nayo yatatutunza.

26

Natamani jamii yenye mgawanyo sawa wa kazi na ushirikiano katika usafi.Wasichana tunachoka sana na kushindwa kujisomea kwa sababu ya kazi nyingi za nyumbani.

27

Kutatua changamoto ya mgawanyo wa kazi nitaandika kitabu na kuigiza mchezo kuhusu mgawanyo sawa wa kazi.Nimechora jamii ambapo wote tunashirikiana na yenye mgawanyo sawa wa kazi za nyumbani ili kila mmoja apate muda wa kusoma.

28

Kutupa taka ovyo kunanichosha. Inaleta kipindupindu na kuharisha.Nitatatua hili kwa kuitisha kikao. Nimechora jamii ya ndoto yangu ambapo watu wanafagia na kutupa taka kwenye dustbin ili tuwe na afya.

29

Kwa kutumia penseli ya miujiza nimechora jamii ya ndoto yangu ina mazingira safi na salama ili kuepuka magonjwa; mfano ugonjwa wa kipindupindu na homa ya matumbo.

30

Jamii ndoto yangu ni ya kusaidiana, mfano kumsaidia mwenzako anapopata ajali barabarani.Inanikwaza kuona watu wazima wakibeba mizigo mizito bila kusaidiwa na watoto wao au wanafunzi wao.

31

Nimechora watoto watiifu wakisaidia watu wakubwa kubeba mizigo. Hiyo ndiyo jamii yenye adabu niliyoichora na penseli ya maajabu.Vitendo hivi vinaleta heshima katika jamii na kuwa na sifa nzuri.

32

Sitaki jamii yangu iwe maskini; jamii ya ndoto yangu nataka iwe na nyumba nzuri, ajira, na elimu kwa wote.Inaniumiza kuona watu wanaokota machupa ili wauze ndio wale. Natamani watu wasome ili wasiteseke.Nimechora jamii yenye shule na ofisi.

33

Kwa kutumia penseli ya miujiza nimechora watu waliopata ajira na wanaishi maisha mazuri. Hamna vibaka kwa sababu kila mtu anafanya kazi.Wanafunzi wanaenda shule na familia zinaishi kwa furaha.

34

Natamani jamii ya ndoto yangu isiwe na ubaguzi wa msichana au mvulana, Tusibague msichana kilema au mwenye ulemavu wa ngozi. Wote wasalimiane na kucheza rede pamoja.Majirani zangu huwacheka walemavu wakipita mtaani. Hilo linanikwaza sana.

35

Nimechora jamii ya ndoto yangu ambapo watu wanapendana na kutobaguana. Nitaenda kwa majirani zangu na kuwaambia kuwa walemavu pia wana haki.

36

Natamani shule zijengwe, miti ipandwe, na mabomba ya maji yawepo.Inanikwaza kuona wavulana wakivuta bangi na kunywa pombe.Jamii ya ndoto yangu nataka watoto wote wasichana na wavulana waende shule wakasome kwa bidii.

37

Penseli yangu ya miujiza imechora wasichana na wavulana wakienda shule kupata elimu na baadae kuwasaidia wazazi wao.

38

Natamani watu wasiharibu miti wala kupoteza maji kwa kuacha mabomba wazi.Takataka na upotezaji wa maji ni kikwazo kikubwa. Natamani baba yangu (ambaye ni mjumbe) anisaidie kukomesha hili.

39

Mchoro wangu kwa kutumia penseli ya miujiza inaonyesha watu wakishirikiana kufanya kazi na hakuna anayetupa taka ovyo wala kuacha bomba wazi.

40

Nataka jamii ya ndoto yangu iwe inavaa stara na isivae mavazi ya uchi si mazuri kwa jamii.

41

Nimechora mazingira yanayopendeza na kuvutia.Ukeketaji wa wasichana unanikwaza sana katika jamii. Natamani ukomeshwe.Kalamu ya maajabu inaonyesha wasichana hawakeketwi bali wanalindwa na mazingira yanapambwa kwa miti na maua.

42

Inaniumiza kuona unyanyasaji wa kijinsia na akina mama wanaochoma watoto wao moto kwa sababu ya kazi za nyumbani.Kalamu yangu ya miujiza itafanya kila msichana aende shule bila hofu ya kubakwa wala kuteswa nyumbani.

43

Inakwaza kuona ndugu akilewa na kumpiga mwenzake bila sababu. Natamani ndoto yangu ya familia yenye amani itimie.Nimechora jamii yenye ushirikiano; mmoja anafagia na mwingine anapanda maua na miti.

44

Mama haniruhusu kwenda shule, ananiambia nibaki nyumbani kufanya kazi wakati wenzangu wanaenda.
Nimechora mtoto analia akichungulia dirishani. Ombi langu kwa wazazi ni kuniruhusu nitimize ndoto zangu shuleni.

45

Inanikwaza kuona vijana wanaharibika kwa kuvuta bangi.Nimechora vijana waliokuwa wanavuta bangi sasa wameacha na wanafanya kazi za maendeleo kwa ushirikiano.

46
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Penseli ya Miujiza: Jamii ya Ndoto Zetu Temeke
Author - Klabu ya Hadithi Zetu-Temeke Klabu ya Hadithi Zetu-Temeke
Illustration -
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs