

Mussa alikuwa mtoto wa pili katika familia yake.
Musa alikuwa mtoto mdogo sana.Alikuwa anapenda sana elimu,muda wote alikuwa achezi na wenzake,alikuwa anakwenda kujisomea chumbani kwake.
Wazazi wake walikuwa wanampenda sana mtoto wao lakini hawakupenda hiyo tabia ya kusomasoma,maranyingi wazazi wake walimgombeza na kumkashifu vibaya.
Mussa mudawote alijisikia mpweke sana.
Japokuwa wazazi wake Mussa hawakupenda hiyo tabia,lakini Mussa alizidi kuwauliza maswali kadhaa,lakini walikaa kimya
Siku moja dada yake kutoka Dodoma alikuja nyumbani kwao.Cha kushangaza alimkuta Mussa akiwa na huzuni.
Aliketi chini polepole kisha akaanza kumuoji mdogo wake kuhusu yaliyo mtokea.Mussa alimueleza dada yake yaliyo mtokea.
Dada yake alihuzunika sana.Usiku ulipofika dada yake Mussa aliwaelezea wazazi wake kuhusu faida ya elimu,lakini wazazi wake Mussa walikataa kumsomesha Mussa.
Dada yake Mussa aliamua kuchukua maamuzi makali,alienda kituo cha polisi na kuwashtaki wazazi wake.Polisi walikubali ombi lake,na kuanza safari ya kwenda kwa kina Mussa,wazazi wake walichukuliwa na kupelekwa polisi wakakanywe.
Walikubali kumsomesha Mussa,na waliporudi nyumbani walimnunulia Mussa winifomu za shule,Mussa alifurahisana, na kuanza shule siku inayofuata. Alikuwa akishika nafasi ya kwanza shuleni,alipendwa na walimu,na wazazi wake pia.

