Sungura na Punda
Josenic Manasse

Hapo zamani za kale, paliondokea wanyama wawili. Mmoja aliitwa Punda na mwingine Sungura.

1

Punda na Sungura walikuwa marafiki wa chanda na pete. Walikuwa wanaishi katika nyumba tofauti.

2

Walikuwa wanasaidiana kufanya kazi zao za nyumbani kisha wakimaliza wanaenda kucheza na kupumzika pamoja.

3

Siku moja walipokuwa wakitembea sungura alimwambia punda, je unajua nyasi ni kijani kibichi punda alikataa na kusema kuwa nyasi ni nyekundu.

4

Sungura alisema basi twende kwa mfalme simba tumuulize na basi punda akakubali.Sungura akamkalia mgongoni kisha wakaenda kwa mfalme.

5

Walipofika kwa mfalme, mfalme alikubali kuwa nyasi ni nyekundu na akasema kuwa sungura atahukumiwa asiongee kwa mwaka mmoja punda alifurahi na kwenda akitabasamu.

6

Hata hivyo punda alivyoenda sungura alimuuliza simba kwanini umenihukumu. Simba akamwambia ni kwa sababu sungura ni mwerevu na anabishana na wanyama wajinga kama punda.

7
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Sungura na Punda
Author - Josenic Manasse
Illustration - , Rob Owen
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs