

Katika Kijiji kimoja kiitwacho Funga Moyo, palikuwa na mwanamme mmoja aitwaye Steve.
Steve alikuwa na mke na watoto wawili. Alikuwa mvuvi wa samaki.
Steve alipopata pesa aliwalipia watoto wake karo ya shule.
Zingine alinunua chakula. Hata hivyo, pesa zake hazikutosha mahitaji yote ya nyumbani.
Siku moja alienda mtoni kuvua samaki kama desturi yake. Kando ya mto palikuwa aa mamba lakini Steve hakumuona.
Ghafla, yule mamba akamrukia Steve na kummeza.
Alipokuwa tumboni mwa mamba alikuwa bado hajapoteza fahamu. Aliona kitu kilichometameta.
Alikichukua na baadaye aligundua kwamba ilikuwa dhahabu.
Alianza kumpiga mateke ili atapikwe Na atoke Na Dhahabu.Yulemamba alisikia kuumwa Na tumbo Na akamtapika Steve.Alibahatika kutoka Na dhahabu Na akachukua kindoo chake cha samaki Na akakakimbia nyumbani.
Alikua Na furaha furifuri alipo karibia nyumbani. mukewe hakumuona Hali YA kawaida ,alimuona Na sura Ya tabasamu na akamuuliza mbona umekawia Na unasura YA tabasamu.
Steve alimwambia mukewe twende nikakuelezee kilicho tokea huko mtoni.Akamuonyesha Ile dhahabu.
Walienda kuiuza Na wakapata pesa na akajenga nyumba kumbwa na akanunua Gari nzito Na akawa tajiri Aliye tajika Kijijini.

