Ndovu mharibifu kijijini
Leah Mahenzo

Kijiji chetu kinaitwa Gotani. Kiko karibu na msitu mkubwa.

Gotani kuna wakulima hodari waliokomaa kama mama yangu.

1

Katika msitu huo ulio karibu, kuna ndovu mmoja mweusi.

Ndovu huyo amekuwa msumbufu kijijini kwa miaka miwili.

2

Wanakijiji waliamua kuchukua hatua kupeleka ripoti kuhusu usumbufu wa ndovu huyo.

Maafisa wa kutunza wanyamapori hawakuchukuwa hatua yoyote kuhusu ndovu huyo mharibifu.

3

Usiku mmoja, ndovu huyo aliingia shambani kwetu.

Aliharibu mihogo yetu iliyokuwa karibu kuvunwa.

Usiku huo alikula mimea yote shambani.

4

Asubuhi ilipofika, mimi na mama yangu tulienda shambani. Tuliona mihogo yetu imetapakaa shambani.

Mama alibaki mdomo wazi na mwenye huzuni mwingi.

5

Mama aliwaza jinsi angekadiria hasara aliyokuwa amepata. Biashara yake ilikuwa imeharibiwa.

Mama alikuwa mkulima na mfanya biashara maarufu sana wa mihogo kijijini kwetu.

6

Baada ya wiki moja, mama na baba waliamua Kumuua ndovu huyo. Walitengeneza mtego ambao ungemdhuru ndovu huyo.

Mtego huo ungemdunga tumboni. Sumu ingeenea miwilini na kusababisha kifo chake.

7

Maafisa wa kutunza wanyamapori walipopata habari hizo, waliamua kumrudisha ndovu huyo kwenye Mbuga ya Wanyama.

Kijiji chetu cha Gotani kiliishi kwa amani.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Ndovu mharibifu kijijini
Author - Leah Mahenzo
Illustration - , Rob Owen
Language - Kiswahili
Level - Longer paragraphs