Ndovu mharibifu kijijini
Leah Mahenzo

Kijiji chetu Kiko Karibu Na msitu mkubwa. Kijiji chetu kinaitwa Gotani. Gotani iko na wakulima hodari waliokomaa kama mama yangu.

1

Katika msitu Huo Kuna ndovu mmoja mweusi. Ndovu Huyo amekua msumbufu kijijini. Amesumbua Kijiji chetu Kwa miaka miwili.

2

Wana Kijiji waliamua kuchukua Hatua kumripoti ndovu huyo. Maafisa wakutunza Wanyama hawakuchukua Hatua yoyote kumhusu ndovu Huyo mharibifu.

3

Siku Moja ndovu Huyo aliingia shambani kwetu. Aliharibu mihogo yetu iliyokua iko Karibu kuvunwa. Usiku huo alikula mimea Yote shambani.

4

Asubuhi ilipofika mimi na mama yangu tulienda shambani. Kufika shambani tuliona mihogo yetu imetapakaa shambani.Mama alibaki mdomo wazi Na huzuni nyingi.

5

Mama alijawa Na huzuni kwani Biashara yake ilikua imeharibiwa.Mama yangu alikuwa mkulima Na mfanya Biashara maarufu wa mihogo Sana kijijini kwetu.

6

Baada ya wiki Moja mama Na baba waliamua Kumuua ndovu Huyo. Waliamua mute ngeneza mtego ambao ungeweza Kumuua ndovu.Mtego huo unge mudunga tumbo lake. Sumu ingetembea kwenye miwili Na angewezawe kufariki.

7

Maafisa wa kutunza Wanyama walipopata habari za mtego, waliamua kumrudisha ndovu Huyo kwenye Pori ya Wanyama. Kijiji chetu cha Gotani kiliishi Kwa Amani.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Ndovu mharibifu kijijini
Author - Leah Mahenzo
Illustration - , Rob Owen
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs