Hadithi ya Sungura na Fisi
Wenworth Maurice
Wenworth Maurice

Hapo zamani za kale walitokea marafiki wawili ambao ni Sungura na Fisi.

1

Siku moja marafiki hao walienda kutafuta chakula, Kwa bahati mbaya walikosa.

2

Sungura na ujanja wake alimshauri Mzee Fisi kwamba wakawale mama zao.

3

Fisi kwa tamaa na upumbavu wake alienda kweli na kumchinja mamake na kumla.

4

Sungura yeye hakufanya hivyo Bali alienda kumficha mama yake.

5

Baada ya Fisi kumchinja na kumla mamake alirudi kwa Sungura na kumwambia kuwa tayari amemla mama yake.

6

Sungura alimcheka Sana,ndio maana mpaka leo Sungura na Fisi ni maadui.

7
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Hadithi ya Sungura na Fisi
Author - Wenworth Maurice
Illustration - Wenworth Maurice
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs