Jinsia katika Jamii Yetu: Changamoto na Suluhisho2
Wanafunzi wa Maktaba ya Jamii Cheche

Sisi ni waandishi chipukizi, wachoraji, na wanaharakati kutoka Maktaba ya Jamii Cheche, Monduli, Tanzania.

Tuliandaa kitabu hiki kuelimisha jamii juu ya changamoto za kijinsia na kutoa mawazo yetu kuhusu namna ya kuzisuluhisha.

1

Katika sehemu hii ya kitabu, tunaangazia baadhi ya changamoto za kijinsia tunazokabiliana nazo katika jamii yetu.

2

Mtoto wa kike anawaza kusoma lakini baba anawaza atakapopata pesa.

Pia mvulana mmoja anawaza kumwoa mtoto wa kike anayewaza kusoma.

Baba anamlazimisha mtoto wa kike kuolewa.

3

Baba anatoka sokoni na mtoto wake. Anamwambia mama, "Mtoto wetu anaweza kuanza kusoma."

Lakini mama anamfokea, "We huoni kwamba ni kilema wa miguu na macho pia."

Mtoto anasema, "Kweli siwezi kuona, lakini nina akili na ninaweza kusikia."

4

Watoto wanafanya kazi ngumu kutokana na ukatili wa kijinsia wa wazazi au walezi.

Kwa mfano, akina mama wengi wa kambo hupenda kutesa watoto. Hii ni changamoto kwa wavulana na wasichana.

5

Baba anamnyima mtoto haki yake. Anamwambia, "Hakuna tena kusoma, kwa sababu wewe ni kilema."

Mama anasema, "Kwa nini unamnyima mtoto haki yake?"

Baba anasema, "Huyu mtoto anatakiwa atafute kazi ya kufanya."

6

Mama anasema, "Nitakushitaki kwa polisi usipomsomesha mtoto." Baba anasema, "Basi nitampeleka shule, lakini akimaliza darasa la saba hataendelea na shule."

Mama anamwambia, "Usipompeleka, nitakushitaki." Baba anasema, "Hata ukinishitaki, simpeleki mtoto shule."

7

Mama mjamzito anafanya kazi nyingi nyumbani. Anapika, anaosha vyombo, pia anambeba mtoto anayelia mgongoni. Mwingine anamshika na kulia pembeni akihisi njaa.

Baba yuko na simu, amepewa chai kwani baba ashibe kwanza halafu wengine baadaye.

8

Huyu kaka anawaza kusoma lakini hajawahi kwenda kusoma.

Anasema, "Baba anampendelea dada lakini sijawahi kwenda shule. Nitakwenda shule."

9

Baba anampiga mtoto bila sababu.

Baba anacheka.

10

Mama anafanya kazi asizoziweza.

Mama anafanya kazi ngumu.

11

Mtoto anaolewa akiwa na umri mdogo.

12

Mtoto mdogo ananyimwa haki ya kusoma au kupata elimu.

Mtoto mdogo anaolewa kabla ya umri wake kufika au kulazimishwa kuozeshwa kabla ya umri.

Mtoto anafukuzwa nyumbani.

13

Mama anamnyima mtoto asiende shuleni afanye kazi za nyumbani.

Mwingine anaenda shuleni.

14

Mama anamshauri baba wampeleke mtoto shuleni kwa sababu baba hataki kumpeleka shuleni. Lakini mama anataka mtoto aende shuleni.

Baba hataki kumpeleka shuleni ili aolewe mapema. Anataka aache shule ili aolewe na baba apate ng'ombe.

15

Katika sehemu hii ya kitabu, tunaangazia baadhi ya mawazo yetu juu ya namna ya kushughulikia changamoto za kijinsia kwenye jamii yetu.

16

Ukiona mtoto anayeomba barabarani, ni bora umsaidie, kama mama huyu alivyofanya.

Alimkuta mtoto anayeomba. Alimchukua na kumpeleka hotelini.

Kisha akaenda kituo cha polisi ili apewe ruhusa ya kuishi naye, halafu akamuarifu mwenyekiti.

17

Hatuna budi kuelimisha watu kupitia makongamano ya kidini na mikutano ya kijamii.

18

Mama amegundua mama huyu anataka kumwachisha mtoto shule. Akamwambia kuhusu madhara ya kumnyima mtoto haki yake ya kupata elimu.

Wanajadiliana kuhusu umuhimu wa mtoto kuendeleza elimu na kutimiza malengo na ndoto zake kama watu wengine.

19

Tunahitaji kuwaelimisha wazazi kutokugombana mbele ya watoto.

Ugomvi baina ya wazazi husababisha mtoto kuwa na msongo wa mawazo na kushindwa kusoma vizuri. Hii inaweza kusababisha mtoto kuacha shule kabisa.

20

Tunatakiwa tuhakikishe watoto wameenda shule ili wapate elimu bora.

21

Mama anamtesa mtoto. Mtoto anakwenda kumshitaki mama yake kwa polisi.

Mama anakamatwa.

22

Kwa kutumia mitandao ya kijamii unaweza kuelimisha jamii na taifa.

23

Tuwasaidie watoto wenye mahitaji maalumu ya shule.

Hivyo tutahakikisha watoto wote wanapate haki yao ya kusoma.

24

Tuwe na ushirikiano katika jamii. Tuwasikilize wanaotoa ushauri. Tunapotoa ushauri wetu tunatakiwa utekelezwe.

Utakuta mtu anataka kusema kitu, ukasema, "Huyu hana cha maana." Kumbe anacho cha maana.

Tuwapende wenzetu. Tusiwe na ubaguzi.

25
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Jinsia katika Jamii Yetu: Changamoto na Suluhisho2
Author - Wanafunzi wa Maktaba ya Jamii Cheche
Illustration -
Language - Kiswahili
Level - Longer paragraphs