Wanyama pori
James Gytrol
Jacob Kono

Kijiji chetu kiko katikati ya mbuga ya wanyama. Wanyama pori huvamia mifugo wetu mara kwa mara.

Wakati wa kiangazi, wanyama pori kama fisi na simba huja vijijini mwetu. Huvamia mifugo wetu zizini.

Uvamizi huu huleta hasara kubwa.

1

Wakati mwingine uvamizi huo huleta maafa au majeraha.

Siku moja, simba alivamia zizi letu usiku na kuwaua mbuzi watatu.

Babangu aliamshwa na kelele za mbwa wetu. Kwa hasira, akachukua mkuki wake kwenda kuokoa mifugo wake.

2

Hakuamini mifugo aliotarajia kuuza ili kupata karo yangu, walikuwa wameuawa. Simba ni mnyama mkali na hatari.

Kabla babangu kukabiliana na huyo adui, nikamwita. "Baba, ninakusihi kabla ya kumshambulia simba naomba unisikize."

3

Nikaomba baba kutomuua simba bali atumie njia mbadala ya kumfukuza. Njia moja ni kama kutumia sauti au mwangaza kuwazuia.

Wanyama pori wana faida na wanapouliwa, hunyima nchi fedha ambazo hutokana na utalii.

4

Baba alinisikiza na akamshtua yule simba kwa kutumia mwangaza na sauti.

Siku iliyofuata, akaenda kuripoti uvamizi huo kwa walinda pori.

Baadaye, akalipwa fidia kutokana na hasara ya uvamizi. Akatumia fedha hizo kujenga ua bora zizini.

5
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Wanyama pori
Author - James Gytrol, John Leshalote, Pauline Lochuman
Illustration - Jacob Kono, Magriet Brink, Rob Owen
Language - Kiswahili
Level - Longer paragraphs