Korongo na Sungura
Anne Kamau
Hesbonah Mogeni

Korongo na Sungura walikuwa marafiki wa kufa kuzikana. Pia, walikuwa majirani wa karibu.

Kila mmoja wao aliishi na familia yake katika boma lake.

1

Urafiki wao ulitokana kwa wao kuonana mara kwa mara wakitafutia jamii zao vyakula.

Kila walipopatana kichakani, waliamkuana na kisha kuendelea kutafuta chakula.

2

Siku moja, Sungura alimualika Korongo kwake na kumuahidi kuwa atamtayarishia supu tamu sana. Korongo alifurahishwa na jambo hilo.

Walitenga siku ya kutembea kwake. Korongo alipofika, alikaribishwa na kuandaliwa supu.

3

Kwa sababu ya mdomo wake mrefu na mwembamba Korongo alijaribu kila njia, lakini hakuweza kuinywa ile supu.

Alihisi vibaya sana kwa kitendo ambacho Sungura alimtendea. Papo hapo akaamua kulipiza kisasi.

4

Hata hivyo alijipa moyo na kumkaribisha Sungura kwake. Siku ya kutembea ilifika.

Sungura hangeweza kupaa juu au kupanda juu ya mti. Waliagana kuwa rafikiye Korongo angembeba kwa mabawa yake.

5

Walipofika nyumbani kwa Korongo, naye alimwandalia supu vile vile. Ilipakuliwa kwenye nyungu ndefu nyembamba.

Sungura alijaribu kuinywa ile supu lakini hakuweza. Mdomo wake haungeingia mle ndani.

6

Sungura alifikiria jinsi ya kufanya ile supu ipande juu. Alimdanganya Korongo kuwa yeye humeza chakula akiwa ardhini.

Alipofika chini aliokota mawe akiyaweka ndani ya nyungu. Hatimaye, supu ilianza kupanda juu na Sungura akainywa. Alifurahi sana.

7

Korongo alipoona hivyo alikasirika na kumkibiza Sungura.

Sungura alikimbia na kuingia shimoni.

Urafiki wao uliishia hapo.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Korongo na Sungura
Author - Anne Kamau
Illustration - Hesbonah Mogeni
Language - Kiswahili
Level - Longer paragraphs