MWANAMIZE
Winnie Mali
Brian Wambi

Hapo zamani zakale,palikuweko na kidosho mmoja kwa Jina Mwanamize.Mwanamize alikuwa msichana mrembo mwenye madaha.Alikuwa na Pua ya kitara, kiuono cha nyigu na Shingo ya upanga.

1

Siku moja, wavyele wake Mwanamize waliondoka kwenda matembezini.wazazi wake Mwanamize walimwambia mwana wao kuwa hawakutaka atoke nje ya nyumba. Mwanamize aliwasikiliza wazazi wake kwa makini na kuwahakikishia kuwa angefuata maagizo.

2

Siku hiyo ,Rafiki zake Mwanamize walifika nyumbani kwa Mwanamize na kumwambia waende kutafuta kuni msituni. Mwanamize alijaribu kukataa lakini rafiki zake walimlazimisha aende nao.

3

Mwanamize aliandamana na marafiki zake kuelekea msituni.Walitafuta kuni hadi jua lilipokuwa likitua ndipo Mwanamize alipokumbuka kuwa alifaa kurudi nyumbani. waliharakisha kurudi nyumbani.

4

Walipofika Karibu na nyumbani Mwanamize alikumbuka alikuwa amesahau mkufu wake msituni. Mwanamize alirudi msituni Kuchukua mkufu wake uliopotea .Kabla ya Kuchukua mkufu wake Zimwi lililokuwalikitisha lilitokea.

5

Zimwi lilimchukua Mwanamize na kumtia Katika ngoma Zimwi lilienda Katika Kijiji cha akina Mwanamize ilikuwa likipiga ngoma Kwa kila nyumba Hulu Mwanamize akiimba. " NI MIMI MWANAMIZE MKUFU WANGU UKAGWA , ZIMWI LIKAJA LIKAMCHUKUA .

6

Bada ya kutembelea nyumba tatu alifika Katika nyumba ya akina Mwanamize. Alipokuwa akipiga ngoma Katika nyumba ya akina Mwanamize wazazi wake waligundua Kuwa Mwanamize ndiye Aliyevkuwa akiimba . wazazi wake waliimpa Zimwi chakula.

7

Walifungua ngoma na kumpata Mwanamize ndani ya ngoma.
Hapo ndipo Mwanamize aligundua kwamba ASIYESIKIA LA MKUU HUVUNJIKA GUU.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
MWANAMIZE
Author - Winnie Mali
Illustration - Brian Wambi, Jesse Breytenbach, Fatma Ahmed, Jacob Kono, Salim Kasamba, Rob Owen
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs