

Hapo zama za kale, paliishi bwana mmoja aliyekuwa mwenye bidii sana. Yeye na mkewe walikuwa wenye umoja na ushirikiano.
Bwana huyo kwa jina Bidii, alikuwa mkulima hodari kijijini mwao, japo familia hii ilikuwa masikini.
Kila siku Bidii pamoja na mkewe, Subira waliamuka asubui na mapema na kwenda shambani.
Bidii alikuwa na shamba kubwa aliloachiwa kama urithi na wazazi wake. Bidii na Subira hawakujaliwa kapata mtoto.
Japo jambo hili liliwasikitisha, hawakufa moyo. Bidii alikuwa mtu mwenye subira na mvumilivu. Alijua kuwa subira huvata heri na mvumilivu hula mbivu.
Alijipiga moyo konde na kujua Maulana ndiye mpaji wa vyote.
Kila kulipokucha, Bidii alianza safari yake ya kwenda shambani. Ilipofika adhuhuri mkewe Subira alimpelekea mmewe chamcha, kidogo alichokipata.
Bidii alishukuru kwani alijua kuwa mtaka vyote hukosa vyote. Alipomaliza kupata chamcha alimshukuru mkewe na kuendelea na kazi.
Siku moja Bidii aliamka asubui na mapema kama ilivyokuwa kawaida yake na kwenda shambani. Alipofika alianza kazi yake.
Mkewe alimletea ujumbe kwamba bwana wawili walitaka kununua mazao yake yote.
Bidii alifurahi sana. Baada ya mauzo hayo alijiendeleza kimaisha.
Hapo ndipo alipojua kuwa bidii hulipa.

