UCHOCHOLE SI KILEMA
PAULINE CHIZI
PAULINE CHIZI

Hapo zamani za kale kuliondokea banati mmoja aliyeitwa Jemima. Alijaliwa kukopolewa katika aila hohehahe ajabu.Kupika na kupakua ilikuwa shida mno.Uchochole uliwanuka kila waendapo.Licha ya uchochole huo,alibahatika kupelekwa Shule.

1

Yeye a likuwa kitinda Mumba.Alikuwa na kichwa chepesi na alifaulu katika mitihani yake.kila siku zilivyozidi kwenda ndivyo Maisha yalizidi kuwa magumu mithili ya ngarange za muvule.

2

Abu yake alipopiga aga dunia ilimulazimu asake vibarua vidogo vidogo.iliaweze kumusaidia Nina yake.Ilimbidi kuacha shule Kwa kipindi fulani.Hakujalilolote alijikazakisabuni.

3

Alijihimiza katika mitihani na hatimaye akamaliza darasa la nane .Matumaini ya kuendelea yalikuwa yamefifia kabisa.Ama kweli mcha Mungu si mfaki.Aliwezakupata mfadili na akayafadhili masomo yake.

4

Alimaliza masomo yake ya sekondari na hata ya chuo kikuu.Maisha ya aila yake yalibadilika.Uchochole haukuwa kilema kwa Jemimah.Aliwezakuwa peleka ndunguze shuleni.Sasa ndunguze wanafuraha lukuki.

5

Aila yake ilinawiri mithili ya waridi.sasa wanajulikana kama mabwenye wanaosaidia maskini.

6

Jemimah sasa hanabudi kumupa Mungu sukurani kochokocho.yeye Ni Mwalimu anayetajika Sasa.

7
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
UCHOCHOLE SI KILEMA
Author - PAULINE CHIZI
Illustration - PAULINE CHIZI, Rob Owen, Jesse Breytenbach, Kenneth Boyowa Okitikpi
Language - Kiswahili
Level - Longer paragraphs