

Zuhura na Wema ni marafiki wakubwa sana. Ni marafiki wanaopendana na kusaidiana.
Leo wamesoma kuhusu jinsi ya kutunza mazingira.
Hivyo wameamua kuanza kutunza mazingira.
Wametambua kuwa utunzaji mazingira ni muhimu sana kwa viumbe vyote.
Watoto wengine wamejumuika kutunza mazingira yao kwa kufanya usafi wa makazi yao.
Pia wanashirikiana na wazazi wao kuhakikisha wanatunza vyanzo vya maji na mazingira yake.
Utunzaji wa mazingira ni muhimu kwa binadamu na wanyama wote. Maji safi na salama ni muhimu kwa afya zetu.
Pia maji ni uhai kwani husaidia kwenye shughuli kama kilimo na ufugaji.
Kilimo husaidia kupata chakula ambacho ni muhimu kwa afya zetu.
Pia hupatia mifugo chakula.
Hata wanyama wa porini hukumbwa na athari kubwa sana pale mazingira yasipotunzwa.
Athari kubwa zilizo dhahiri ni kama upungufu au ukosefu wa mvua.
Ni vyema watoto wajue kuwa kuna faida nyingi za kutunza mazingira.
Je, utunzaji mazingira una faida gani zaidi?

