Nyuki waleta balaa
Njeri Wachira
Unsplash Website

Amani na familia yake waliishi shambani mwao.

Nyumba yao iliyokuwa imejengwa kwa mbao, ilipendeza sana.

1

Mama Amani alipenda maua na miti kwa hivyo alipanda kwa wingi.

Nyuki walipenda kunywa nekta ya maua ya mama Amani.

2

Nyuki walipenda kujenga kwenye kuta za nyumba.

Wazazi wa Amani walijua wangevuna asali baada ya miezi kadhaa ingawa walielewa hatari ya nyuki.

3

Mwaka baada ya mwaka baba Amani alijihami kwa mavazi spesheli ya kujikinga na nyuki.

Alivuna asali tamu kwa wingi. Alihifadhi asali ndani ya chupa mbalimbali.

4

Walitumia asali katika chai, mkate na mandazi. Hawakuhitaji sukari ya dukani.

5

Pia walitumia asali kama dawa. Kila wakati mtu alipokohoa, mama Amani alichanganya asali na kiini cha yai.

Alimpa mgonjwa vijiko viwili, akisema, "Kunywa hii itakusaidia."

6

Mara kwa mara Amani alidungwa na nyuki.

Sehemu aliyodungwa, ilivimba na kuuma.

7

Lakini siku moja kukawa na janga. Mamake na babake Amani walienda mjini kununua bidhaa za kutumiwa pale nyumbani.

Watoto waliachwa nyumbani wakicheza.

8

Mtoto mmoja alianguka karibu na mzinga, nyuki wakakasirika. Wakatoka kwenye mzinga na kudunga chochote walichokipata.

Waliwadunga watoto, bata, ndama na kuku.

9

Wazazi waliporudi waliwapata watoto wakiwa wamedungwa na nyuki. Mdomo wa Amani ulikuwa umevimba vibaya.

Bata watano walikuwa wamekufa tayari. Baba aliwachukua watoto na kuwapeleka hospitali.

10

Kumbe nyuki anatufaa lakini anaweza kuleta balaa!

11
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Nyuki waleta balaa
Author - Njeri Wachira
Illustration - Unsplash Website, Njeri Wachira
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs