Kofia ya maajabu
Mustafa Ibrahim and Conquerors Primary school
Rob Owen

Hapo zamani za kale, palikuwa na kijana aliyeitwa Kiongozi. Kiongozi alikuwa mtoto wa Kwanza na wa kipekee wa Mzee Shangari.

Kiongozi alikuwa mtoto mtulivu na alimsaidia baba yake kuuza kwenye duka lao kubwa.

1

Siku moja, rafikiye Musa, alikuja kununua kofia. Alimwambia Kiongozi amtafutie kofia nzuri ya kupendeza.

Kiongozi alimwuliza, "Unaenda wapi na kofia hii unayotaka kununua?"

Musa alimwambia, "Mimi na familia nzima tunaenda mjini."

2

Humo dukani hapakuwa na kofia. Kwa furaha, Kiongozi alienda katika chumba cha baba yake. Aliichukua kofia aliyoipenda sana Mzee Shangari na kumpa Musa.

Musa alienda nyumbani akiwa amejawa na furaha tele moyoni mwake.

3

Mzee Shangari aliporudi jioni, aligundua kwamba kofia yake haikuwepo.

"Mwanangu, umeiona kofia yangu ya maajabu?" aliuliza Mzee Shangari.

"Ndiyo baba, nilimpatia rafiki yangu Musa," alijibu Kiongozi.

"Eti nini?" Mzee Shangari alianguka.

4

Mzee Shangari alikuwa amepewa kofia hiyo na baba yake. Ile kofia ilikuwa imebeba bahati yake ya maisha.

Kwa hivyo, haikufaa kupatiwa mtu mwingine isipokuwa tu mtoto wake.

5

Angempokeza mtu mwingine ile kofia kungetokea bahati mbaya na kufanya familia kuangamia.

Kusikia hivyo, Kiongozi alikimbia haraka na kumpa Musa kofia nyingine. Alimwomba babake msamaha.

6

Mzee Shangari alianza kumuelezea mwanawe kuhusu ile kofia ya maajabu. "Watu walioichukua bila kujua, walipata madhara na kuugua maradhi yasiyopona."

Mzee Shangari aliendelea kumsimulia jinsi babake aliaga dunia.

7

"Babu yako alikuwa Mzee mwenye kufanya miujiza."
Mzee Shangari alichukua kofia ile na kuiombea ili isisababishe madhara yoyote.

Kutoka hiyo siku, Kiongozi alikoma kutenda jambo lolote bila kuulizia mawaidha.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Kofia ya maajabu
Author - Mustafa Ibrahim and Conquerors Primary school
Illustration - Rob Owen
Language - Kiswahili
Level - Longer paragraphs